Posts

RAIS MAGUFULI ATEUA WANNE, NI WAKURUGENZI NA WENYEVITI.

Image
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi ameeleza kuwa Rais Magufuli amemteua   Prof. Lazaro S.P. Busagala   kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki ( TAEC ) kuanzia tarehe 22 March, 2018. Prof   Lazaro S.P. Busagala  alikuwa Makamu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara ( CBE ) kitivo cha Taaluma na Utafiti. Prof. Damian Gabagambi ameteuliwa  kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa ( NDC ) kuanzia tarehe  22 March, 2018 .  Prof. Gabagambi   anachukua nafasi ya Mlingi Elisha Mkucha ambaye atapangiwa kazi nyingine.  Kabla ya uteuzi Prof. Gabagambi   alikuwa Mhadhiri wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Kilimo, Sokoine ( SUA ). Rais Magufuli  amemteua   Dkt. Deodatus Michael Mutasiwa   kuwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma. Dkt. Alphone Bilola ameteuliwa  kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma.  Kabla ya Uteuzi huu Dkt. Chandika alikuwa...

VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO 24/3/2016

Image

ZALTAN ATIMKIA LA GALAXY YA MAREKANI

Image
Gwiji wa soka wa Sweden   Zaltan Ibrahimovic  aliyekuwa akiitumikia   Man United  ya  Uingereza  ametimkia nchini Marekani kattika clabu ya LA GALAXY ya nxhini Marekani . Kikubwa na kilichowashangaza wengi ni style ya kipekee aliyoitumia kuutangazia umma kuwa kwa sasa anaenda kucheza soka Marekani . Zaltan amenunua ukourasa mzima wa gazeti la LA TIMES na kuandika tangazo maalum la ujio wake katika ligi ya MLS. Zaltan amatimka Man united na takwimu zifuatazo.                Mechi alizocheza --------59                Assist                   ---------10                Magoli                  ---------29

TRUMP KUWA SHAHIDI MBELE YA MWENDESHA MASHITAKA MAALUM

Image
Rais wa Marekani Donald Trump ameonyesha nia ya kutoa ushahidi mbele ya mwendesha mashitaka maalum anayechunguza uingiliaji kati wa Russia katika uchaguzi mkuu wa Marekani wa mwaka 2016 na mambo mengine. Ningependa -Trump alijibu alipohojuiwa na waandishi wa habari kutaka kujua kama ana nia ya kuhojiwa na wachunguzi. Rais alitoa jibu hilo wakati akiondoka katika chumba cha kidiplomasia cha White house mara tu baada ya kusaini nyaraka ya kuelekeza utawala wake kuchukua hatua za kibiashara dhidi ya China. Majibu ya Trump yalikuja baada ya taarifa kwamba mmoja wa mawakili wake John Dowd kuthibitisha kwamba anajitoa.

ROLI LAUA WAWILI SEKENKE

Image
Kutoka mkoani Singida  muda huu nitaarifa yalori la mafuta lililoanguka na kutumbukia darajani na kisha kuwaka moto katika eneo la   sekenke   na watu wawili wanaripotiwa kupoteza maisha. Kamanda wa polisi mkoa wa  Singida   Deborah Magiligimba  amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba watu wawili wanasadikiwa kupoteza maisha japo majina yao bado hayajatajwa.

STARS YACHABAGWA 4-1

Image
Timu ya Taifa ya Tanzania imetndikwa kwa mara nyingine tena na timu  ya taifa ya Algeria katika mchezo uliomalizika wa kirafiki uliopigwa nchini Algiers. Mchezo huo wa kirafiki umemalizika kwa Tanzania kuchabangwa  4-1, magoli ya Algeria ya metiwa kimiyani na Bounedja Baghdad aliyefunga mawili, Shomari Kapombe akajifunga moja, na Carl Menedja akafunga la 4, goli la kufutia machozi la Tanzania lilifungwa na Simon Msuva. : Mara ya mwisho Tanzania ilipokutana na Algeria - Taifa Stars ilikubali kipigo cha 7-0

ENEO LA BIASHARA HURU LA BARA LA AFRICA KUUNDWA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini makubaliano ya kuunda eneo la Biashara Huru la Bara la Afrika. Makubaliano hayo yamefikiwa katika m kutano uliowakutanisha viongozi wa umoja wa Africa mjini Kigali nchini Rwanda. Tanzania iiwakilishwa na waziri mkuu Mh Kassim Majaliwa.